Social Icons

Monday, September 24, 2012

FIESTA 2012 IRINGA HII HAPA

 
Lina mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya Bongofleva kutoka kundi la THT akicheza na Tausi mmoja wa mashabiki waliojitokeza katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012, linalofanyika kwenye uwanja wa Samoramjini Iringa ambapo wasanii mbalimbali wanafanya vitu vyao jukwaani wakiburudisha mashabiki wa mkoa wa Iringa, Lina ameweza kufanya mambo makubwa na kuwaimbisha mashabiki wake ukizingatia kwamba anatoka mkoa huo
 
Meneja Masoko wa kampuni mya Push Mobile Rugambo Rodney akitangaza washindi wawili wa pikipiki walioshinda habati nasibu hiyo katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012 mjini Iringa kwenye uwanja wa Samora  huku wasanii mbalimbali wa muziki wa Bongofleva wakionyesha uwezo wao katika muziki na kukonga nyoyo za mashabiki waliofurika kwenye uwanja huo, katika picha aliyeshika kipaza sauti ni mtangazaji wa Clouds Fm, B12.
 
Meneja Masoko wa kampuni mya Push Mobile Rugambo Rodneyakipiga picha ya pamoja na mmoja wa Ali Mohamed Sanga kazi wa Msindo Iringa mjini ambaye ni  mshindi wa moja ya  pikipiki
 
Amini akiimba jukwaani katika tamasha hilo
 
Mkali wa muziki wa R&B Ben Paul akikamua jukwaani kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa.
 
Msanii Rich Mavoko akiwa ameruka hewani wakati akicheza pamoja na wanenguaji wake jukwaani katika tamasha la Serengeti Fiesta mjini Iringa.
 
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Linex akiimba kwa hisia kali jukwaani katika onesho la muziki la Serengeti Fiesta kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa , msanii huyo mwenye uwezo wa kutawala jukwaa amefanikiwa kukata kiu ya mashabiki wa muziki wake.
 
Wadau kutoka duka maarufu la nguo mjini Iringa  wakishoo Love katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012 kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa ktoka kulia ni Sadok aka Isadow, Eric aka Ricrose na Gasper aka G Star, duka lao linaitwa Perfect Classic Wear .
 
Shabiki  wa muziki wa bongofleva anayejulikana kwa jina la Tausi akicheza  na rafiki yake  vilivyo  katika tamasha hilo.
 
Dj PQ akifanya vitu vyake kwenye mashine wakati wasanii wakiimba jukwaani kazi yake kubwa ni kucheza CD za wasanii hao wakati wakiimba jukwaani.
 
 
Rachel akimwaga mauno jukwaani ametisha kwa ujumla mjini Iringa na mashabiki wamemkubali.
 
Msanii Sundy Gaga akifanya vitu vyake  jukwaani katika tamasha la Serengeti uwanja wa Samora
 
Mshindi wa Serengeti Fiesta Super Nyota kutoka mkoani Mbeya anayejulikana kwa jina la Ney Lee akiimba jukwaani kwenye onesho la Serengeti Fiesta linalofanyika  kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa.
 
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Bongofleva anayekulikana kwa jina la Young Killer akifanya vitu vyake jukwaani  huku
 
Hapa ni Full Kushangweka mwenye kurusha juu ngua haya, mwenye kitambaa mkononi haya mwenye koti haya ilimradi burudani imekolea.
 
Nyomi la mashabiki waliofurika kwenye uwanja wa Samora kwa ajili ya kushuhudia tamasha la Srengeti Fiesta 2012 mjini Iringa.
 
Wasanii chipukizi kutoka mkoani Iringa wakiimba jukwaani katika shoo ya utangulizi kabla ya wasanii maarufu kupanda jukwaani katika tamasha la Serengeti Fiesta linalofanyika kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa. 
Mashabiki wakifuatilia kwa karibu wakati wasanii chipukizi kutoka mkoani Iringa wakifanya vitu vyao jukwaani.
 
Mashabiki wamejitokeza kwa wingi ili kushuhudia kitakachofanyika katika onesho hilo ni full mzuka kwenye uwanja wa Samora 
Msanii huyu naye alimekamua vilivyo jukwaani

No comments:

Post a Comment