Social Icons

Saturday, November 10, 2012

SHETTA KUMTOA 'BONGE LA BWANA' MWISHO WA MWEZI

Msanii kutoka pande za Ilala anayetamba na hits kama “Mdananda” na “Nidanganye” along side Diamond Platnumz, Nurdin Bilal Ally alias Shetta sasa yupo mbio kuja na ujio wake mpya baada ya kutamba na ngoma zake hizo.

Latest infoz kutoka kwa Shetta zinasomea kuwa ifikapo November 25 ya mwaka huu ataachia ngoma yake mpya kwa jina la “Bonge la Bwana“. Single yake hiyo mpya amempa collabo mkali toka Tanzania House of Talent {THT} mwanadada Linah. Baada ya kusema hayo aliongeza kwa kusema ngoma hiyo mpya ataitambulisha rasmi ndani ya New Maisha Club siku ya November 25, baada ya hapo ndipo itaanza kwenda rasmi katika vituo mbalimbali vya Radio. Hii chini ni mmoja ya tweet ya Shetta ikiwa ni taarifa juu ya ujio wa ngoma yake hiyo mpya

No comments:

Post a Comment