Social Icons

Wednesday, December 5, 2012

NASSA AWACHANA MASTAA WA MOROGORO

 
Siku chache baada ya kuvum ahewani kwa kideo ch angom ayake ya Awali iliyopewa jin ala 'Kila Nabii'mkali kutoka mji kasoro bahari Morogoro,Nassa tayari amechia kitaani ngoma nyingine kali aliyoibatiza jina la Mastaa ambayo ndani yake amewachana vilivyo nyota kutoka mji huo kwa madai kuwa wamekuwa wakifanya kazi kubwa kujitangaza wenyewe tofauti na kuutangaza mkoa wao kama wanafanya nyota kutoka Arusha.
Katika Interview aliyofanya na mchomvuink,Nassa amesema kuwa inaweza kuwa vigumu kwa watu kumuelewa kutokanana na hiki anachokisema lakini ukweli utabaki kuwa wasanii kutoka Moro hawafanyi kazi kubwa kuutangaza mkoa kama ilivyo kwa watu wa kaskazini.

"Ni kweli wapo waliofanya lakini bado naona ni kwa kiwango kidogo sana, si kama ambavyo wamekuwa wakitumia nguvu kubwa kujitangaza wenyewe, nataka kuliondoa hilo na mwisho wa siku nitakuwa wa kwanza kuitangza Moro na kuwafunika wakongwe wote, ambao wako bize na kujitangaza wakiwania shoo za hapa na pale" alisema

No comments:

Post a Comment