Social Icons

Wednesday, December 5, 2012

SIRI YA KIMYA CHA MORACKA HII HAPA

Moracka kushoto akiwa na M. Kadinda
Ni kitambo sasa mkali wa  'Crank' Bongo, Mohamed Hassan Mo Racka amekuwa  kimya jambo ambalo limekuwa likizusha nong'ono za hapa na pale kuwa  huenda  nyota huyo kafulia  kimuziki.
 
Kupitia  mchomvuink pekee stori iliyopo ni kuwa Mo anataraajia kukusanya mamilioni ya mkwanja kupitia matangazo ya kampuni moja kubwa hapa nchini dili ambayo kwa asilimia kuwa ndiyo ilimfanya kushindwa  kufanya jambo lolote kwenye  gemu ya  Bongo fleva.
 
"Nitakupigia baada ya siku mbili uje kucheki mkataba wa mamilioni ambao ninatarajia kuusaini na kampuni moja kwa ajili ya matangazo, hilo ndiyo jambo lililokuwa  linanifanya kuwa bize, nafikiri bada ya hapo nitakuwa poa  kufanya kazi zangu za muziki kama kawaida" alisema  Mo

No comments:

Post a Comment