Social Icons

Thursday, December 13, 2012

TUNAHITAJI WAREMBO GANI KWENYE VIDEO ZETU?


kulikuwa na maneno mengi sana ya chichini mara  baada ya kutolewa kwa  video ya wimbo 'Baadae' wa  mkali wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz ambayo kama wengi wanavyofahamu  kichupa chake kiligongwa nje ya nchi.
kama  ndiyo kwanza  unasoma sentesi hii  unaweza kujiuliza  juu ya hicho ulichokisoma  hapo juu,  lakini ukweli ni kuwa  nong'ono zilizokuwepo ni kuhusiana na  msichana aliyetumika  kwenye kichupa hicho kuonekana ni wa kiwango cha kawaida  pengine kuliko hata  warembo waliopo hapa nchini.

Taarifa  zilizopo ni kuwa  Ommy  alitumia  kiasi kikubwa cha fedha kusafiri mpaka nchini Afrika Kusini tayari kwa kufanya  video hiyo huku pia  akitumia  mamilioni kumlipa  msichana huyo ambaye  licha  ya kubeba  sifa ya mmoja  wa  model maarufu nchini humo lakini bado hakuonekana  kukidhi kiu ya watazamaji wa kichupa  hicho

Hapo ndipo swali  linapokuwa  tunahitaji warembo wa kiwango gani kuzifanya video zetu kuwa za kuvutia  zaidi, najiuliza ni wapi alipo Eliza   yule aliyeshiriki  kwenye video ya Bob Junior Oyoyo, ama  ni wapi alipo yule binti aliyeonekana kwenye video ya Binti Kiziwi , si hao tu na  imani kuna wengine wengi, sasa  kama ni hivyo kun ahaja gani ya kusafiri mpaka ng'ambo kwenda kumchukua mtu ambaye uzuri wake haufanani hata na yule mwanamke mpenda sifa  anayetangaza kipindi fulani cha runinga  hapa nchini.

 majibu tutayaona kupitia Comments zenu

No comments:

Post a Comment